Kampuni ya Western Digitial inayomiliki biashara ya memori kadi za
SanDisk wametambulisha memori kadi hii mpya ya ujazo wa GB 400
katika onesho la IFA 2017 linaloendelea huko Berlin, Ujerumani
SanDisk wametambulisha memori kadi hii mpya ya ujazo wa GB 400
katika onesho la IFA 2017 linaloendelea huko Berlin, Ujerumani
Baada ya uzinduzi wake ni muda mfupi inatarajiwa kuingia sokoni kwa
kiasi cha Dola za Kimarekani zipatazo 250 (Takribani *Tsh 560,000).*
Sifa ya memori kadi hii ni kwamba ina spidi ya UHS-1 yaani inaweza
kusafirisha 100MB/s ambapo ni sawa na picha 1,400 kwa dakika moja. Pia
inaweza kuhifadhi video ya masaa 40 yenye kiwango cha 1080p.
Memori kadi hii itawasaidia watumiaji Simu Janja na Kamera kuwa na uwezo
mzuri kuhifadhi vitu vingi kwa wakati mmoja.