12.2.17

Jinsi Ya Kurudisha Picha Zilizofutika Katika Smartphone Yako

BY net tamaduni


Kuna wakati inatokea unafuta picha zako kwenye simu yako kwa bahati
mbaya au hata kuna muda to unataka kurudisha picha zako ulizowahi
kuzifuta kutoka kwenye simu yako kama unataka kufanya hayo yote basi
usijali kwani leo tutaenda kujifunza namna rahisi ya kurudisha picha
zako hizo kwenye simu yako kwa namna rahisi kabisa.
Hata hivyo kama inavyojulikana watu wengi sana wanajua namna ya
kurudisha picha zilizopotea kwenye kompyuta lakini watu wengi hawajui
kufanya hivyo ikija katika swala zima la Smartphone au (Android Phones)
au hata simu nyingine za mkononi, hivyo basi leo tutajifunza hatua kwa
hatua namna ya kufanya hivyo bila kutumia muda mwingi.

Kwa kuanza basi iii kuweza kufanikisha hili unahitaji kuwa na bando
atlist MB100 kwaajili ya kupakua programu kutoka kwenye PlayStore, pakua
Programu ya Android iitwayo (DiskDigger) bofya hapo chini kupakua
programu hiyo ya android kwenye simu yako.

Baada ya hapo install programu hiyo kisha ruhusu programu hiyo kupitia
superuser baada ya hapo chagua file lenye picha zilizo potea alafu
chagua format kama ni jpg, png au hata mp4 kisha acha programu hiyo
ifanye scaning baada ya hapo moja kwa moja utaweza kurestore picha zako
na hata video.