31.3.16

FAHAMU MAMBO 5 YA KAMPUNI YA APPLE AMBAYO PENGINE HUYAJUI

BY net tamaduni

Karibu Net TAMADUNI.Katika miaka 40 ya Apple yapo matukio mengi na mambo mengi ambayo yamefanyika lakini sio yote yanajulikana zaidi, makala hii itakuletea mambo ambayo hayajulikani saana kuhusu apple. 


*1.Mjue Ronald Wayne ambaye ni mmoja ya waanzilishi wa kampuni ya
Apple.*

Ronald aliuza share zake za apple kwa dola za kimarekani 800 mda mfupi

tu baada ya yeye na wenzie kuanzisha kampuni ya Apple, inasemekana

kwamba alifanya hivyo baada ya kuhofia kwamba iwapo Apple wangeshindwa

kibiashara basi mali zake zingebinafsishwa.

Wasichojua wengi kuhusu Ronald Wayne ni kwamba anajihusisha na mahusiano

ya watu wa jinsia moja, na alimwambia habari hii Steve jobs wakati bado

wakiwa waajiriwa kabla hawajaaanzisha kampuni ya Apple.

Ronald anasema hajutii kuuza hisa zake Apple wiki chache baada ya

kuanzishwa, anadai kwamba aliyafanya maamuzi hayo kwa kutegemea taarifa

aliyokuwa nayo kipindi kile . Yeye ndiye mbunifu wa logo ya kwanza

kabisa ya Apple.

*2. Steve Jobs aliuza gari lake ili aweze kutengeneza kompyuta ya
kwanza ya Apple* 

Pesa ambazo ziligharamia utengenezwaji wa Kompyuta ya kwanza ya Apple

ambayo ilikuwa inajulikana kama */Apple computer 1/* ama */Apple 1/*

zilitokana na pesa zilizokusanywa baada ya Steve Jobs kuuza usafiri wake

wa pekee wa */VW mini bus/* na Steve Wozniak kuuza calculator yake ya

/*HP-65*/

Jobs aliuza usafiri wa pekee ili kulipa gharama za kutengeneza kompyuta

ya kwanza, gari hilo lilikua kama hili.

*3. Kompyuta ya kwanza ya Apple ilichukua siku kumi tu*

Baada ya kuwa na pesa kwa ajiri ya kutengeneza kompyuta iliwachukua

/Apple/ siku kumi kukamilisha kazi. Kompyuta hiyo ikauzwa kwa dola za

kimarekani */666.66/* Wozniak anasema hakuwa anajua chochote kuhusu

mambo ya kishetani kuhusishwa na namba hiyo kwa wakati huo hivyo hiyo

namba haina uhusiano wowote na imani za kishetani.

*4. Steve Jobs aliwahi kushwa cheo akaamua kwenda kuanzisha kampuni

nyingine.*

Mwaka 1985 Steve Jobs alishushwa cheo cha umeneja na bodi ya wakurugenzi

baada ya kutokea kugombea madaraka katiyake na aliyekuwa mkurugenzi

mtendaji wa wakati huo, Jobs akaondoka na baadhi ya wafanyakazi

wakaanziasha kampuni ya *NEXT.*

Hata hivyo mkurugenzi mtendaji aliyesababishwa kuondoka kwa Jobs Apple

alisababisha hisa kushuka na hivyo akaondolewa na baada ya muda

akaajiriwa mtendaji mwingine ambaye alimrudisha Jobs Apple kwa kununua

kampuni ya NEXT. Tukisheherekea miaka 40 ya Apple tujifunze kutoka kwa

mwanzilishi wake Jobs ambaye hakukata tamaa aliposhushwa cheo katika

kampuni yake.

*5. Apple walishawahi kuwa na pesa nyingi kushinda serikali ya Marekani*

Kwa kipindi kifupi mwaka 2011 Apple walikuwa wanahifadhi ya pesa kubwa

hata kushinda hifadhi ya pesa ya Serikali ya Marekani, Hii ilitokana

hasa na ukubwa wa madeni ya Marekani kwa wakati huo.

Yako mambo mengi ambayo hayajulikani kwa watu hasa watumiaji wa bidhaa

za Apple hayo matano ni ni machache ambayo mimi ninmepata kuyafahamu,

wakati tunasheherekea miaka 40 ya Apple.